vote

Sheikh Mkuu wa Tanzania apatikana


Sheikh Aboubakar Zuberi.


Baraza kuu la waislamu Tanzania (BAKWATA) asubuhi ya leo lamteua Sheikh Aboubakar Zuberi kuwa Mufti mpya wa muda.

Hatua ya uteuzi huo inafuatia kifo cha aliyekuwa Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti, Issa Shaaban Bin Simba aliyefariki kutokana na  shinikizo la damu na kisukari katika Hospitali ya TMJ na kuzikwa mkoani Shinyanga wiki iliyopita.

Sheikh Zuber atashikilia nafasi hiyo kwa muda wa miezi mitatu (siku 90) kuelekea katika uchaguzi wa kumpata atakayerithi nafasi hiyo kwa mamlaka kamili.

Chanzo: Hivi Sasa
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog