vote

JK ateuliwa mjumbe AU




Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete, ameteuliwa kuwa mjumbe mpya wa umoja wa Afrika AU kwenda nchini libya akichukua nafasi ya Mohamed Dileita aliyeshika nafasi hiyo tangu mwaka 2014.

Uteuzi huo uliofanywa na Umoja wa Afrika katika kikao chake kilichofanyika jijini Addis Ababa nchini Ethopia kimeleza uteuzi huo ni   sehemu ya juhudi za umoja huo kuhikisha usalama unarudi nchini libya.

Kamishina wa Amani na usalama wa AU,Smail Chergui jana alitangaza uteuzi huo alipokuwa anatoa muhtasari wa majadiliano na makubaliano ya kikao hicho kilichiwakutanisha viongozi wa ngazi za juu wa nchi wanachama.

Chanzo: Hivi sasa
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog