vote

Rais Kikwete ataja sifa za ‘mrithi’ wake

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.


Rais Jakaya Kikwete ametaja sifa za  mrithi wake kufuatia  hatua za mwisho kumaliza utawala wake uliodumu kwa muda wa miaka kumi.

 Akibainisha sifa za mtu anayetakiwa kuteuliwa na kamati kuu mbele ya wajumbe   wa Halmashauri Kuu ya CCM  amesema  kamati hiyo  haina budi kumchagua mgombea urais anayekubalika ndani na nje ya chama hicho.

Kikwete amesema hayo wakati akifungua kikao cha Halmashauri Kuu kwenye ukumbi wa ofisi ya makao makuu ya chama hicho mkoani Dodoma

“Watanzania wote bila kujali itikadi zao wanaitazamia na kuitumainia CCM kutoa uongozi ulio bora kwa nchi yetu. Hali hii inathibitisha uleusemi wa Baba wa Taifa kwamba Rais anaweza kutoka chama chochote lakini rais bora atatoka CCM,” alisema.

Ameongeza kuwa   wakimpata mtu ambaye  CCM inampenda, lakini wananchi hawatampenda, chama hicho kitaumia, dhana ya kuwa wakichagua mtu yoyete mradi katoka CCM, watakuja kukiona cha mtema kuni.

Aidha, kamati kuu CCM   ipo  katika  mchakato  wa kumpata mgombea mpya baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wake wa vipindi viwili vinavyokubalika kikatiba, huku kukiwa na ongezeko kubwa la nguvu ya upinzani.

Hata hivyo Kamati Kuu ya CCM imewaachia huru makada wake sita waliotumikia adhabu ya miezi 17 ya kuzuiwa kujishughulisha na shughuli za uchaguzi baada ya kubainika kukiuka sheria za uchaguzi za chama hicho kutokana na kuanza kampeni mapema.

Makada  waliangukiwa na adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja ni pamoja na mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye.

Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba na Mbunge wa Sengerema,  William Ngeleja.

Uchaguzi mkuu wa Rais pamoja na wabunge mwaka huu unatarajia kufanyika wiki mwisho ya mwezi oktoba kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

 Chanzo: Hivi Sasa
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog