vote

Uchaguzi 2015: CUF kutikisa Zanzibar, Chadema yaambulia jimbo moja


Katibu Mkuu Chadema Dk Wilbroad Slaa  (kushoto) pamoja na Viongozi wakuu wa UKAWA: Prof. Ibrahim Lipumba na James Mbatia.

Kinyang’anyiro cha Ubunge mwaka 2015 visiwani Zanzibar, Chama cha Wananchi (CUF)  kinatarajia  kusimamisha wagombea wake wa nafasi ya ubunge katika majimbo yote ya uchaguzi visiwani Zanzibar,  huku Chadema ikiambulia  jimbo moja  la Kikwajuni.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa CUF, Omar Ali Sheikh, amesema Ukawa wamekubaliana   CUF kuchukua majimbo  yote    isipokuwa  katika Jimbo la Kikwajuni watasimamisha mgombea ubunge kutoka Chadema ambaye ni Salum Mwalimu.

Aidha, Mwalimu ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar). Jimbo la Kikwajuni linaunganisha wakazi wa maeneo ya Kikwajuni Juu na Chini, Kisimamajongoo, Kilimani, Miembeni, Magereza na sehemu ya eneo la Michenzani na hadi sasa linamilikiwa na Hamad Yussuf Massauni (CCM), ambaye pia ni mzaliwa wa eneo la Kisimamajongoo.

Hata hivyo watafiti wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba  Mwalimu amezaliwa na anatoka katika familia yenye makazi katika eneo maarufu la Kisimamajongoo.

Wakazi wa eneo la Kisimamajongoo wanaaminika ni ndugu wa damu hivyo  huenda likawa ni moja ya jambo litakalowavutia wananchi wa jimbo hilo kuweka kando tofauti zao za kisiasa na kuamua kumpa uongozi Mwalimu.

Chanzo: Hivi Sasa
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog