Wapinzani wa Yanga kwenye
michuano ya Kombe la Shirikisho
Afrika, Etoile du Sahel
wamewasili jijini Dar es Salaam wakiwa tayari kabisa kuivaa Yanga kesho
Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wakiwa kwenye uwanja wa ndege
wachezaji wa kikosi hicho cha Tunisia walionekana wako tayari kuivaa Yanga,
kesho.
Msafara wao uliongozwa na
Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka la Tunisia (FTF), Krifa Jalel, akiwa na
Rais wa Etoile du Sahel, Charefeddine Ridha, wachezaji 19, benchi la ufundi
lenye watu 13, waandishi wa habari 12 na wanachama 10.
Taarifa zimeeleza Etoile
itafikia katika Hoteli ya Ledger Plaza, zamani ikijulikana kwa jina la Bahari
Beach eneo la Kunduchi, ambapo leo Ijumaa jioni inatarajiwa kufanya mazoezi
katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Waamuzi wa mchezo huo ni
Samwel Chirindiza, Arsenio Marenguka, Celio de Jesus Musabe, Jose Maria Bachide
wote kutoka nchini Msumbuji na wanatarajiwa kuwasili leo mchana, huku kamisaa
wa mchezo huo, Salah Ahmed Mohamed kutokea nchini Sudan akitarajiwa kuwasili
leo jioni na wote walitarajiwa kufikia katika Hoteli ya Protea iliyopo
Oysterbay.
Post a Comment