vote

EFG yatoa Mafunzo kwa wanawake wafanyabiashara wa sokoni zaidi ya 100 jijini Mwanza

Baadhi ya wanawake wafanyabiashara wa sokoni wakiwa katika kongamano hilo jijini Mwanza

Baadhi ya wanawake wafanyabiashara wa sokoni wakiiimba kwa furaha katika kongamano hilo jijini Mwanza

Wafanya biashara wa soko la mkuyuni wakijitambulisha katika kongamano hilo

Baadhi ya wanawake walioshiriki katika kongamano hilo jijini hapa






Mkurugenzi Mtendaji wa Equality For Growth(EFG), Jane Magigita akitoa mafunzo kwa wanawake wafanyabiashara walioshiriki kongamano hilo.









ZAIDI ya  wafanyabiashara wanawake 100 mkoani hapa, jana walipatiwa mafunzo ya kukuboresha ushiriki wao, katika shughuli  za kimaendeleo hususa kumwezesha, kutafakari kwa kina tatizo la umasikini na kuweka mikakati thabiti ya kukabiliana nalo.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kongamano la kwanza la wanawake wafanyabiashara sokoni Tanzania lililofanyika Kwenye  ukumbi wa  Mwanza  Hoteli ,  Mkurugenzi wa bodi ya watendaji wa shirika la Equality for Growth (EFG), Emmanuel Tuju alisema, lengo ni kumwezesha mwanamke kutumia zaidi mali, nguvu na jitahada ili kujiletea maendeleo na kulinda haki zao katika umiliki wa mali.

Tuju alisema, sera iliyopo katika sekta isiyo rasmi inawapa wanawake mwongozo wa serikali unaolenga kuwapa  wananchi mwelekeo wa maendeleo unaohakiki  mipango na mikakati  inazingatia usawa wa jinsia kila sekta.

 “Kutokana na hili sisi kama Equality For Growth tumeamua kuleta elimu hii nchi nzima kwa kuanzia mikoa saba ambayo ni Mwanza, Tanga, Shinyanga, Lindi, Mtwara,Mbeya na Dar es salaam, ili  kuhakikisha mfanyabiashara mwanamke anapata haki ya kumili mali zake”.

Mkurungezi mtendaji wa EFG Jane Magigita alisema, wanawake wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo kutokuwepo na sheria inayosimamia haki zao  kutokana na  mapungufu makubwa yaliyopo, utashi thabiti wa viongozi serikalini pamoja na sera kutumika kisiasa zaidi ya maendeleo.

Alisema ili kuinua maendeleo ya sekta hii, viongozi wanapaswa  kutunga sheria  na kuzisimamia kwa ajili ya  kuboresha miundombinu pamoja na kutoa fursa, haki sawa kwa wananchi walio katika sekta hiyo.

Aidha baadhi ya washiriki wa kongamano hilo ambao pia ni wafanyabiashara wa sokoni walisema, wanakumbana na changamoto mbalimbali zikiwemo za utozwaji wa ushuru sawa na wafanyabiasha wakubwa.

 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wafanyabiasha Soko la Mkuyuni Veneranda Joseph  alisema, Halmashauri imeshindwa kutofautisha wafanyabiashara wadogo na wakubwa wakati wa  kuwatoza ushuru kwani wote  wanalipa kiwango sawa.

 Naye Mwenyekiti wa Soko Kuu mkoani Mwanza Ahmed Nchola alisema, ni vema halmashauri ikatenga   eneo husika kwa wafanyabiashara wanaopanga bidhaa zao chini, kwani wengi wao hawaliipi kodi kama wanavyolipa wa maduka na meza.

Hatahivyo biashara ndogondogo huzalisha ajira kwa watu million 2.4 kwa mwaka huku watu 440,000 huingia katika sekta isiyo rasmi  hawa hujumuisha wahitimu wa darasa la saba, waliopunguzwa kazi, wastaafu na wahitimu kutoka vyuoni.

 





Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog