vote

Uchaguzi wa Rais Sudan kuanza leo


Uchaguzi mkuu  nchini Sudan umeanza leo , huku Rais wa sasa Omar Al Bashir akitarajiwa kushinda.
Takriban wapiga kura milioni 13 watakuwa wakimchagua Rais na wabunge 450. Huku vyama vya upinzani vikisusia uchaguzi huu vikidai hautakua huru na wa haki.

Katika vituo vya kupigia kura wapiga kura wachache wamefika huko ilikutekeleza wajibu wao wa kikatiba. Vyama vingi vya upinzani vimesusia uchaguzi huo kutokana na kile vinavyodai kuwa ukandamizaji wa kisiasa unaoendeshwa na rais Omar al Bashir.

Wagombea 15 wanaoshindana na Bashir kwenye uchaguzi huo inadaiwa kuwa  hawana uwezo mkubwa na wengine hata hawajulikani kote nchini Sudan.

Huu ndio utakaokuwa uchaguzi wa kwanza tangu Sudan Kusini ijitenge 2011. Matokeo yanatarajiwa kutangazwa Aprili 27
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog