vote

Baraza la Wawakilishi kuichambua Bajeti Zanzibar


Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mh. Pandu Ameir Kificho akiambatana na Makatibu na walinzi wa Baraza hilo.

Baraza la Wawakilishi Zanzibari linatarajia kukutana   siku ya jumatano mei 13 kujadili Bajeti ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa mwaka  fedha wa  2015/2016.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Baraza la Wawakilishi Yahya Khamis Hamad amesema kwamba Wajumbe wa Baraza hilo watapata nafasi ya kujadili Bajeti hiyo ambayo ndio mwelekeo mzima wa shughuli zote za kiserikali. Katika mkutano huo jumla  ya maswali  81 yataulizwa na kujibiwa.

Ameongeza kuwa fursa hiyo ni muhimu kwa wajumbe hao kuitumia vyema kujadili mambo ya msingi yanayowahusu wananchi badala kujadili mambo yasiyo na tija kwa wananchi.

Kwa upande mwingine Yahya amesema  katika kikao hicho pia Miswada miwili ya sheria itawasilishwa na kujadiliwa ikiwemo mswada wa Sheria ya Fedha na Mswada wa sheria wa kuidhinisha matumzi ya serikali kwa mwaka 2015/2016.
 Chanzo: Hivi Sasa
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog