vote

FPCT: Vijana ibueni miradi ya maendeleo




WANACHI na wakazi  wa Jiji la Mwanza, wametakiwa kutotegemea serikali peke yake, badala yake kuongeze bidii katika kuhakikisha wanaibua miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi ili kukuza uchumi.

Wito huo umetolewa jana na Mratibu wa Shirika Lisilo la kiserikali MWAOMI,  linalohudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na utunzaji wa Mazingira  Fredrick Eliakim alipokuwa akifungua maadhimisho ya sherehe ya  siku ya mtoto wa Afrika ambayo hufanyika Juni 16 kila mwaka,

alieleza kuwa, serikali peke yake haitaweza kutekeleza mahitaji ya watanzania wote bila ya wananchi wenyewe na mashirika binafsi kuonesha umuhimu wao katika jamii inayo wazunguka.

“Serikali haiwezi kufanya kila kitu bali inahitaji kuungwa mkono na mashirika binafsi yenye uwezo kifedha katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa”alisema Eliyackimu.

Alieleza kuwa,shirika hilo lililoko chini ya uongozi wa  Kanisa la Free Pentecostal Church of Tanzania(FPCT),limekuwa na mchango mkubwa kwa serikali kupitia Nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na Elimu, Afya, na Utunzaji wa mazingira katika shule za msingi  zilizopo kata ya Buswelu wilayani Ilemela.

Sherehe hizo, znazofanyika jijini hapa katika uwanja wa shule ya msingi Kahama, zilishirikisha wadau mbalimbali wa Elimu wilayanmi humo ikiwa ni pamoja na walimu na wanafunzi kutoka katika shule nane ambazo ni Lukobe,Masemele,Kisabo, Igogwe, Nyamwilekelo, kahama na kabusungu, zote za kata ya Buswelu.

“Tumefanya sherehe hizi kwa kushirikiana na walimu wote lengo likiwa ni kuwajengea watoto kukua katika Nyanja mbalimblai ikiwa ni pamoja na Kijamii,Kisaikolojia, Kimwili,Kiakili na pia kihisia” alisema.


sambamba na hilo Maadhimisho hayo yaliambatana na michezo mbalimbali kutoka katika shule hizo, ikiwani njia moja wapo ya wanafunzi kudadilishana mawazo katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu, mazingira na mambo mengine ya kuwajengea uwezo wanafunzi .

Afisa elimu na mzingira wilayani humo Benatus Kahulu aliyemuwakilisha Mkurugenzi wa manispaa hiyo John wanga alisema aliupongeza uongozi wa shirika hilo kwa kazi nzuri wanayo ifanya ya kuhakikisha inasaidia Jamii ya wana Ilemela bila kujali dini wala kabila.

 Mratibu wa idara ya Michezo kutoka katika Shirika la MWAOMI Dicksoni  Juma, alieleza kuwa, wameamua kuanza mashindano hayo mapema, ili kuwaandaa watoto vizuri na katika kuhakikisha siku hiyo wanaifikia wakiwa na furaha kutokana na ushirikiano uliopo wa shule hizo za msingi .

Alieleza kuwa kupitia mashindano hayo, Shirika limeandaa zawadi mbalimblai kwa washindi  ambazo watakabidhiwa Siku ya tarehe 16 Juni ambayo itakuwa ni siku ya mtoto wa Afrika Duniani, hivyo aliwataka walimu na wanafunzi kutoa ushirikiano wao wa dhati katika kuhakikisha sherehe hizo zinamalizika kwa amani na utulivu.

“sisi tumejipanga katika kuhakikisha mashindano haya yanakamilika kwa wakati muafaka, hivyo ni jukumu la walimu na wanafunzi wenyewe kuona umuhimu wa mashindano haya ambayo huleta umoja, ushindi na mshikamano baina yao”alisema Dickson.

shule zitakazoshiriki mashindano hayo kuwa ni pamoja na Lukobe,Masemele,Kisabo,Igogwe,Nyamwilekelo, Kahama, Kabusungu na ,Kilabela na  kwamba timu itakayo shinda katika kinyang’anyilo hicho, itapata zawadi ya Kombe, jezi na mpira kwa  mshindi wa kwanza, na mshindi wa pili na watatu watapata zawadi ya jezi na mpira.

Mashindano hayo, yalifunguliwa na mechi mbili kati ya shule ya msingi  Nyamwilolelwa na kabusungu, ambapo upande wa mpira wa miguu shule ya msingi nyamwilolewa  iliibuka  kidedea kwa bao 6-0 dhidi ya kabusungu huku mpira wa pete nyamwilolelwa ikishinda mabao 30 dhidi ya kabusungu ilioambulia bao 3. 





Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog