vote

Vijana watakiwa kujiunga na mchezo wa Judo



Baadhi ya wanafunzi wa mchezo wa judo katika chuo cha Shotokan Karate wakifanya mazoezi jana, katika uwanja wao uliopo Igoma Jijini Mwanza.


JAMII imetakiwa kuuchukulia mchezo wa Judo (Karate) kama michezo mingine ya kuimarisha viungo na kuondokana na dhana iliyopo ya kuwa mchezo huo ni ugaidi.

Akizungumza na BINGWA jana, Mwalimu wa Judo katika chuo cha Shotokan Karate, Amri Khasani alisema kuwa jamii inatakiwa kuelewa kuwa mchezo wa Judo ni sawa na michezo mingine ya kuimarisha Afya.

“Mchezo huu wa Judo kwa hapa Mwanza hauna kipaumbele sana kutokana na jamii kuuchukulia tofauti, lakini nikuhakikishie kuwa hakuna mchezo mzuri kama huu kwa kuwa unaimarisha mwili kwa asilimia kubwa” alisema Khasani.

Kwa upande wake Nasoro Suleimani anayecheza Judo alisema anashangazwa na vijana wengi wa Mwanza kwa kutokujiunga na Mchezo huo kwa kuwa unawaepusha na mambo mengi ya kihuni.


“Mchezo huu nimeucheza tangu mwaka 1977, nakumbuka siku moja nimempeleka mke wangu Hospitali kujifungua usiku wakati narudi nikavamiwa na wezi lakini nikawakabili na kumkamata mmoja wao, kama sikuwa na mazoezi wangenimaliza” alisema Suleiman.

Hata hivyo Suleiman aliitaka Serikali kutoa kipaumbele kwa mchezo huo kwa kuwa unaweza kuisadia kuwa na vijana wengi walio imara.




Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog