vote

BARAZA LA WAZEE MAGU LAOMBA SERA YA WAZEE ITUNGIWE SHERIA









BARAZA la wazee la Kata ya Magu mjini, Kitongosima na Lumeji lenye Jumla ya wazee 150, limeiomba serikali itungie sheria sera ya wazee ya mwaka 2003.

Pia wameomba  kutengewa chumba  chao maalumu kwaajili ya matibabu katika zahanati, vituo vya Afya,Hospitali za Wilaya,mikoani na Hospitali za Rufaa nchini.

Wakizungumza na uongozi wa shirika la MAPERECE kupitia viongozi wa mabaraza wazee hao walieleza kuwa, sera ya wazee imekaa mda mrefu bila kutungiwa sheria na hivyo kuwa fanya wazee kukosa maamuzi yakudai haki zao kama ilivyo ainishwa katika sera ya wazee ya mwaka 2003.

Hermenegid   Mganga, ni Katibu wa Balaza la wazee kata ya Magu mjini ambaye alieleza kuwa kuwepo kwa sheria hiyo, kutawasaidia wazee kupata haki zao bila kuwa na matatizo yoyote  katika upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa wazee.

Angizungumzia suala la Afya kwa wazee, Mganga aliiomba serikali kutenga vyumba vya matibabu kwaajili ya waze kutokana na baadhi ya wilaya kutotekeleza  huduma za matibabu bure kwa wazee.

“sisi kama wazee, tunaiomba serikali itutengee na sisi vyumba maalumu kama walivyotengewa  wanawake wajawazito na kliniki za watoto ili tupate huduma za Afya kwa utaratibu unao faa” Alisema Mganga.

Hata hivyo alieleza kuwa, katika kuhakikisha hilo, ni vema serikali ikatambua umuhimu wa miundombinu na huduma za Afya kwa wazee na kuziboresha kwani vituo vingi havina  sehemu ya kusubilia matibabu na kwamba wanapofika katika vituo huhitaji sehemu ya kukaa na kupumzika wakisubilia huduma.

Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog