vote

Hong Kong kujadili mageuzi ya kisiasa







Baraza la kikatiba la Hong Kong limeanza kujadili mpango wa mageuzi ya kisiasa kabla ya kupigiwa kura baadaye wiki hii.

Mapendekezo yao ni kuwa wakaazi wa Hong Kong wataweza kumpigia kura kiongozi wao katika uchaguzi wa mwaka wa 2017 japo wagombea wote kwanza lazima waidhinishwe na serikali kuu ya China .

Watetezi wa demokrasia wameshutmu hilo kuwa demokrasia ya longo longo.

Tayari mamia ya watetezi hao wamekusanyika nje ya afisi za baraza hilo wakibeba mabango na kutoa maneno ya kutukana baraza hilo.

Lakini wanaoungamkono mpango huo kutoka Beijing wanasema kuwa Hong Kong kwa sasa inahitaji uthabiti na wametoa wito kwa wabunge hao wapitishe pendekezo hilo.

Chanzo: Hivi sasa
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog