vote

MKATABA WA MESSI HAUJACHAKACHULIWA

Add caption




KLABU ya Simba imekanusha tuhuma za kuuchakachua mkataba wa winga wake, Ramadhani Singano 'Messi' kama anavyodai.



Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya klabu hiyo yaliyopo Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini hapa jana mchana, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Hajji Manara, amesema klabu inatambua mkataba wa Messi wa miaka mitatu unaomalizika mwakani na si mwaka huu kama anavyodai winga huyo.



"Habari hizi ni upotoshwaji, Simba haijachezea mkataba wa Messi kutoka miaka miwili na kuwa mitatu, Messi ni mchezaji mdogo sana. Naambia hao mawakala uchwara, waache kumvuruga. Hii ndiyo staili yangu ya leo," amesema Manara.



"Tunaomba TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) walitolee ufafanuzi suala hili badala ya kukaa kimya kwa sababu taswira ya Simba inachafuka," amesema zaidi Manara aliyeonekana kufura kwa hasira.
Chanzo: Mpenja Blog
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog