Polisi nchini Kenya wanazuilia mashua moja inayoshukiwa kuwa na madawa ya kulevya.
Aidha
watu watano wamekamatwa baada ya kupatikana na kilo mbili za mihadarati
aina ya heroin, huku raia mmoja wa Uingereza akisakawa kujibu maswali.Msako huu ulianza wiki iliyopita baada ya polisi kupata ripoti ya ulanguzi wa madawa ya kulevya mjini Kilifi, kilomita 70 Kaskazini mwa Mombasa.
Polisi waliliandama gari moja dogo hadi Bandari ya Kilifi
Kwa mujibu wa Mkuu wa Polisi mjini Mombasa, bwana Robert Kitur, gari hilo lilipatikana na kilo mbili za madawa ya heroine, iliyo na thamani ya karibu dola 65,000.
''tulivizia gari moja ambayo tulikuwa na ufahamu kuwa ilikuwa na walanguzi wa madawa ya kulevwa na tulipoipekua tulipata kuwa walikuwa na karibu kilo 2 za Heroin'' alisema afisa mkuu wa polisi wa Mombasa Robert Kitur.
Inaaminika kuwa madawa hayo yalikuwa yasafirishwe hadi Kisiwa cha ushelisheli au mjini Dar-es-Salaam .
Post a Comment