vote

Mbowe aweka ‘ Kizingiti ’ ACT kujiunga UKAWA


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

Mpango wa Chama cha ACT-Wazalendo kujiunga UKAWA umeuka kuwa kaa la moto kufuatia Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe kutamka bayana kuwa hawatamruhusu Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, kujiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Aidha, akihojiwa na Waandishi wilayani  Kyerwa Mbowe amesema hawamwamini tena Zitto kwa madai kuwa akiingia Ukawa atakuwa akivujisha siri za umoja huo kwenda Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kauli ya Mbowe imetolewa  baada ya Zitto kutangaza kuwa ACT ipo tayari kujiunga na Ukawa kama wanavyotaka Watanzania. Chama cha ACT-Wazalendo  kilitangaza kuwa kipo tayari kushirikiana na vyama vingine vya siasa kwa lengo la kuleta mapinduzi ya uchumi na kubomoa mfumo unaowanyonya wananchi.

Katika hatua nyingine, Chama cha ACT-Wazalendo kujiunga na Ukawa huenda ikawa ni ndoto isiyokuwa na majibu  huku shauku ya kushirikiana na vyama vingine ikiteketea.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog