vote

Ugonjwa usiojulikana wavamia Babati mkoani Manyara


Na Wolter John, Babati

Wakazi  wa kijiji cha matufa kitongoji cha Burunge kata ya magugu Wilaya ya Babati mkoani  manyara wameingiwa   hofu kubwa kutokana na kuibuka  kwa ugonjwa ambao haujafahamika mpaka sasa.

Akizungumza na Mwandishi wa Blog hii mwenyekiti wa  kijiji cha  cha burunge  kata ya matufa, Ramadhan Mangi ameeleza kuwa mpaka sasa ugonjwa huo  haujafahamika na  umeua watu wawili wa familia moja huku wengine watano wakiwa bado wanaendelea na matibabu katika kituo cha afya cha Magugu.

Asha Shabani ni mmoja ya waathirika wa ugonjwa huo  na ambaye pia  baba yake amefariki kutokana na ugonjwa huo ameeleza kuwa alianza kujisikia vibaya na kukosa hamu ya kula  na baada ya muda kidogo alianza kutapika,  kuharisha na alipopelekwa hospitali alitibiwa na alipotaka kujua anaugua ugonjwa gani daktari hakuweza kumjibu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji cha Burunge Dismas Baranda  amesema kuwa ugonjwa mpaka sasa una muda wa wiki mbili na kila mgonjwa anapoenda kupima huambiwa ni homa ya matumbo kitu ambacho kinaleta hofu kubwa kutokana na ugonjwa huo kuendelea kusambaa kwa wengine.

Madaktari  wa  kituo cha afya  magugu   wamewaeleza wakazi hao  hawana maabara ya kuweza kupima na hivyo  wamepeleka vipimo katika maabara ya  hospital ya mkoa ya Arusha ya  Mount Meru kwa ajili ya kupata majibu.

Hata hivyo wakazi hao wameshauriwa kutumia maji safi yaliyochemshwa, kula vyakula vya moto,kutoshikana mikono, kuchimba matundu ya vyoo pamoja na kuwapatia vidonge maalum ili kujikinga na ugonjwa huo.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog