vote

Tucta yahamasisha Uchaguzi Mkuu






Wafanyakazi wa umma na sekta binafsi jijini Mwanza wameshauriwa kujiandikisha kwa wingi kwenye daftari la wapigakura ili waweze kuwachagua viongozi bora katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Chama cha Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Yusuph Simbaulanga, alisema kura ni nyenzo muhimu inayoweza kuepusha malalamiko yasiyo ya lazima yanayoweza kujitokeza baada ya uchaguzi.

“Idadi ya watu wanaojiandikisha imeongezeka, hivyo kwa fursa hii ni vyema pia wafanyakazi kujiandikisha kwa wingi kwani wengi ni vijana wanaofanya kazi katika sekta binafsi na za umma,” alisema Simbaulanga.

Aidha, alisema kujiandikisha kwa wafanyakazi kutawafanya kuoana thamani ya kura zo katika kufanya uamuzi sahihi wakati wa Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.

“Kupitia sanduku la kura mfanyakazi ataweza kujikomboa kwa kuchagua viongozi watakaoleta tija kwenye utendaji, lakini pia kuboresha maslahi yao,” aliongeza Simbaulanga.

Alitumia nafasi hiyo pia kuwahimiza
wafanyakazi kuhudhuria maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) mwaka huu itakayofanyika kitaifa jijini Mwanza ili kushiriki pia kupima afya zao kuhusu magonjwa ya kisukari, shinikizo la damu na ukimwi, ambapo wataalamu wa afya watatoa vipimo hivyo bila malipo.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yanayoratibiwa na chama cha wafanyakzi wa migodini, nishati na ujenzi (Tamico) chini ya Tucta ni Rais Jakaya Kikwete.

Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog