vote

Zitto: ACT – Wazalendo tunauzika


Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe



Kiongozi mkuu wa Alliance for Change and Transparency (ACT - Wazalendo), Zitto Kabwe, amewaomba Watanzania kupima sera na matendo ya viongozi wa chama hicho kujiridhisha kwamba kinafaa kuwaletea maendeleo ya kweli.

Zitto alitoa kauli hiyo wakati akihutubia mkutano wa hadhara mjini Musoma, Mara, hivi karibuni, akisema wananchi wana hiari ya kujiunga na chama chochote cha siasa wanachoona kinawafaa.

Akifafanua zaidi, Zitto aliwaomba wananchi kumpima vitendo vyake kutokana na uvumi unaosambazwa na baadhi ya watu kwamba ni msaliti wa kisiasa.

Alisema wanasiasa kutofautiana ni jambo la kawaida, hasa mtu anapopigania masilahi ya wananchi katika jumuiya ya wanasiasa wengi.

Zitto umefika wakati wa kufanya siasa za maendeleo badala ya kutumia majukwaa ya siasa kumtukana mtu au chama kingine.

“Kinachotakiwa ni mwanasiasa kusimama jukwaani na kuwaeleza wananchi atakachowafanyia iwapo watawachagua na siyo kutukanana kwani wananchi wana kiu na maendeleo na siyo kutukanana matusi,” alisema Zitto na kuongeza:

“Hivi ukigombana na mke wako ndani halafu ukaenda kijiweni kuwaeleza wenzako kuwa tumegombana na mke wangu ndani na ukawaeleza sababu za kugombana ni nani atakayeonekana mjinga, mke wako au wewe uliyeenda kuwaeleza?”

Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Anna Mghwirim, alisema siasa ni maisha, hivyo wanasiasa wanaochezea maisha ya wananchi hawastahili kukabidhiwa uongozi wa umma.

Alisema chama hicho kimekuja na misingi thabiti ya kuinusuru nchi inayolemewa na mzigo mkubwa, hasa wa ukosefu wa ajira kwa vijana wengi.

“Taifa kwanza leo na kesho ili kurudisha misingi yote iliyokuwepo ambayo kwa sasa haitumiki, lengo ni kurudisha matumaini kwa wananchi,” alisema.

Share this article :

Post a Comment

 
Support : GUDMUSICS BLOG | Gm Template | Gm Template
Copyright © 2015. NGOWI HABARII - All Rights Reserved
Template Created by 0756494700 Published by GM Template
Proudly powered by gudmusics blog