![]() |
Mh, Edward Lowassa |
Kwa mujibu wa wachambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Tanzania wameiambia hivisasa blog kwamba katika matembezi hayo Lowassa amewaondoa hofu wananchi na kudhihirisha kuwa afya yake iko safi kutokana na kudaiwa kuwa na matatizo ya afya huku wengine wakisema hawezi kuhimili mikimiki ya kampeni na shughuli nyingine zinazohitaji nguvu.
Matembezi hayo yalianzia barabara ya Mandela, Kilwa kupitia Temeke Mwisho, Wiles, Temeke Hospitali, Chang’ombe Polisi, Kiwanda cha Bia cha Serengeti na kuhitimishiwa viwanja vya TCC.
Akizungumza baada ya kuhitimisha matembezi hayo yaliyoandaliwa na kikundi cha Temeke Family Sport Club Lowassa ameitaka Serikali kuongeza jitihada katika uhamasishaji na kupinga mauaji hayo.
Katika hatua nyingine Lowassa ameitaka jamii kutambua kuwa albino ni sawa na watu wengine na wasitengwe kwa sababu nao wana haki ya kuishi kama watu wengine.
Post a Comment